Vifo hivyo vilizuka baada ya maelfu ya watu kusongamana kwenye lango la hekalu walipokuwa waking’ng’ania kuingia ndani nyakati za alfajiri katika mji wa Deogarh ulioko mkoani Jharkhand.
Watu hao 11 waliofariki walikuwa wamelala usiku nje ya lango la hekalu kwa lengo la kuwatangulia wenzao kuingia ndani asubuhi iliyofuatia.
Watu hao wanaojumuisha wanawake 8 walifariki baada ya kukanyagwa na wenzao waliokuja asubuhi, huku wengine 24 pia wakiripotiwa kujeruhiwa katika tukio hilo.
Sherehe hiyo ya kitamaduni iliyokuwa na umuhimu mkubwa katika imani ya Wahindi inatarajiwa kuendelea kwa mwezi mmoja.