Mechi za kombe la dunia la FIFA 2018 zitachezwa kwenye viwanja 12 vilivyokuwa katika miji 11 nchini Urusi.
Mechi ya ufunguzi, nusu fainali moja na fainali zitachezwa kwenye uwanja wa Luzhniki ulioko mjini Moscow nchini Urusi. Mechi ya nusu fainali nyingine itachezwa mjini Saint Petersburg.
Ratiba ya mechi za mashindano ya Confederation Cup ya mwaka 2017 pia ilibainishwa siku ya Ijumaa.
Mji wa Saint Petersburg ndio utakaoandaa mashindano ya Confederation Cup ya mwaka 2017 nchini Urusi.