Mara baada ya onyesho hilo, Chris alipanga kuondoka nchini humo siku ya Jumatano kwa ndege yake binafsi kuelekea Hong Kong kwa ajili ya onyesho jingine.
Lakini serikali ya Ufilipino ilitoa tangazo kwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Manila kutomruhusu Chris kuondoka mpaka atakapolipa deni lake.
Deni hilo amatakiwa kuwalipa wadhamini ambao walimuandalia tamasha kali kipindi cha mwaka mpya, ingawa Chris hakutokea kwenye show hiyo.
Lakini Brown mwenyewe aliandika katika akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Twitter, "Sijui chochote kuhusiana na mambo yanayotendeka sasa. Nilikuja hapa kufanya onyesho kama malipizo ya onyesho nililolikosa kipindi cha mwaka mpya. Na nimeshafanya onyesho hilo siku tatu zilizopita".