Header ads

Header ads
» » Waziri wa Ulinzi Korea Kaskazini Auawa Baada ya kuchapa Usingizi Mbele ya Rais

Taarifa hiyo iliyotolewa bungeni imesema Hyon Yong-Chol alipigwa na kombora la kuangusha ndege mbele ya mamia ya maafisa wakuu serikalini
Idara ya ujasusi ya Korea Kusini imesema kuwa waziri wa ulinzi wa Korea Kaskazini ameuawa kwa kutokuwa muaminifu kwa kiongozi wa nchi hiyo, Kim Jong-un.
Taarifa hiyo iliyotolewa bungeni imesema Hyon Yong-Chol alikutana na mauti yake baada ya kupigwa kwa kombora la kuangusha ndege mbele ya mamia ya maafisa wakuu serikalini mwishoni mwa mwezi Aprili.
Bwana Hyon anasemekana kuwa alisinzia katika hafla iliyokuwa ikihutubiwa na rais Kim jambo lililomuudhi sana kiongozi huyo wa kiimla.
Hata hivyo ukweli wa ripoti hiyo haujabainika kutokana na usiri wa serikali ya Korea Kaskazini.Waziri wa ulinzi wa Korea Kaskazini ameuawa kwa kutokuwa muaminifu kwa kiongozi wa nchi hiyo, Kim Jong-un.
Bwana Hyon alipandishwa cheo na kuwa Generali mwaka wa 2010 na kuuawa kwake kunatia shaka udhabiti wa uongozi wa rai Kim Jong -un.
Hyon alipandishwa cheo na kutangazwa kuwa waziri wa usalama wa taifa mwaka uliopita.
Mwandishi wa BBC aliyeko huko Seoul anasema mauaji hayo ya kikatili mbele ya umma ikiwa yatathibitishwa, yanaonyesha athari za uasi dhidi ya Kim Jong-un.
Mapema idara hiyo ya ujasusi ilisema viongozi wakuu katika serikali ya Korea Kaskazini wamekuwa wakiuawa kila mmoja kwa wiki.Chang alikamatwa katika mkutano wa hadhara na kupelekwa katika eneo la hadhara alikouawa
Mara ya mwisho kwa kiongozi huyo wa korea kaskazini kuamrisha kuuawa kwa kiongozi mkuu serikalini ilikuwa ni mwaka wa 2013 alipoamrisha ami wake
Chang Song-thaek - kukamatwa na kutiwa kitanzi.
Chang alikamatwa katika mkutano wa hadhara na kupelekwa katika eneo la hadhara alikouawa mbele ya umma.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post