Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetoa msaada wa mabati 850 ikiwa ni ahadi iliyotolewa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, kusaidia waathirika wa mafuriko katika kijiji cha Mwakata wilayani Kahama.Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa (pichani), alisema msaada huo una thamani ya Sh. milioni 12.Dk. Slaa alifafanua kuwa kati ya kiasi hicho cha fedha zilizonunua mabati, Sh. milioni 10 ni sehemu ya ruzuku inayotolewa na serikali kwa chama hicho na kiasi kingine ni michango iliyopatikana katika mikutano ya hadhara ya chama hicho iliyofanyika mjini Kahama.Alisema waliamua kununua mabati hayo kutokana na kamati ya mkoa inayoratibu maafa hayo ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Ally Rufunga, kupendekeza vinunuliwe vifaa vya ujenzi kutokana na chakula kuwapo cha kutosha.
Dk. Slaa aliwataka viongozi kuhakikisha wanasimamia vema ujenzi wa nyumba za kuduma za makazi ya wananchi wa kata ya Mwakata kama ilivyopendekezwa na Rais Jakaya Kikwete, alipotembelea waathirika hao kwani mara nyingi serikali imekuwa ikishindwa kutekeleza kwa wakati majanga kama hayo.“Niwaombe viongozi wa mkoa kusimamia waathirika hawa wajengewe nyumba kwamuda mwafaka…
Watanzania wengi tanawakatisha tamaa kutokana na kushindwa kutimiza ahadi zinazotolewa kama kule Kilosa hadi leo bado watu wanaishi kwenye mahema, tangu nikiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, naomba sana Shinyanga muwe wamfano,” alisema Dk. Slaa.
Katika hatua nyingine, misaada imeendelea kutolewa kwa waathirika hao baada ya Kampuni ya Simu (TTCL), kutoa chakula na vitu mbalimbali vyenye thamani ya Sh. milioni tatu.Meneja wa TTCL Mkoa wa Shinyanga, Peter Kuguru, alisema kampuni yake imeungana na Watanzania wengine walioguswa na maafa hayo kutoa msaadawa kibinadamu na kuyaasa mashirika mengine na watu mbalimbali kujitokeza kuwasaidia wananchi hao.
Topics: MATUKIO
Imehaririwa na;- Unknown
Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
Playstore
TeknoTaarifa Video
TAARIFA ZILIZOSOMWA SANA
-
Wachezaji wa Yanga wakifanya mazoezi jana jioni kwenye uwanja wa Mbegani, Bagamoyo Timu ya Yanga SC jana imekamilisha kujifua kwa m...
-
BEST TANZANIAN UNIVERSITIES 2015: Latest Rankings 23 February 2015. A list of best universities has just gotten out and the result i...
-
WATU wawili, Said Abdallah (37) na Ally Mwishee (44), wameuawa kwa kupigwa risasi na kufa papo hapo katika uwanja wa mpira wa miguu wa ...
-
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA Kumb. Ref. Na EA.7/96/01/H/41 ...
-
mabingwa hao watetezi wa ligi kuu ya Premia ya Uingereza walipokuwa wakikabiliana na Swansea jana usiku huku wakiwa na mchezaji mmo...
-
Kama ndo machine aliyo nunua safari hii basi katisha aisee maana hii ni one of the most expensive and luxury cars around na hela ya...
-
The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) is a Government Institution which is under the Ministry of Education and Vo...
-
He trusts lions enough to stick his arm in their mouth! Kevin leverages his ability to help prevent these...
-
JOB VACANCY Precision Air Services Plc is a fast growing private Tanzanian airline which operates in Partnership with Kenya Air...
-
Mshambuliaji matata wa Barcelona na kapteni wa Argentina Lionel Messi,...