Kamanda wa Polisi Singida, Thobias Sedoyeka amesema Jeshi la Polisi linamshikilia mwanamke mmoja kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mjukuu wake ambapo alimtupa mtoto huyo kwenye dirisha la basi ambalo lilikuwa kasi, mwanamke huyo Waridi Saidi alimtupa mtoto huyo akiwa kwenye basi namba T 981 ALS la kampuni ya Salumu Classic lililotoka Dar kwenda Kigoma.
Mama huyo alimtupa mtoto huyo kijiji cha Iguguno, wilaya ya Mkalama alimtupa mjukuu wake Mayasa Meshaki, Dk Adamu Hussein amesema
walimpokea mtoto akiwa katika hali mbay kutokana na kuvuja damu nyingi
na siku ya pili alifariki dunia kutokana na jeraha la kupasuka kwa
fuvu la kichwa.
Lawaridi amesema; “dirisha
lilikuwa wazi yani nilimshusha tu nikamchukua Mayasa nikamtupa bila
kutegemea… Watu wakanivamia sasa huku wanapiga kelele kuanza kunipiga…
Wamenipiga sana tu, basi gari ikasimama wakawa wameenda kumtafuta mtoto…
nikaambiwa mtoto amepatikana lakini mpaka dakika hii sijamuona...“
Kuisikiliza taarifa hiyo wakati ikiwa inarushwa na ITV bonyeza download hapa.