Header ads

Header ads
» » KILABU YA WATOTO YAFUNGULIWA MJINI NEW YORK

 Children dance during an electronic dance music party at a night club in New York on October 26, 2014 
028 FilipWolak Cirkiz 9189
Kilabu ya watoto walio kati ya umri wa miaka 6 na 12 ilifunguliwa rasmi katika mji wa New York wilaya ya meatpacking nchini Marekani.
Mgahawa huo unaomilikiwa na kampuni ya Cirkiz utakuwa ukifunguliwa mara moja kila mwezi kuwapa watoto fursa ya kujivinjari mbali na vifaa vya kiteknolojia vilivyomo majumbani mwao.
Laura lampart aliyekuwa ameandamana na mwanawe alisema kuwa kilabu hiyo ina manufaa kwani watoto walijihisi kama watu wazima na hakukuwa na tatizo la kuhofia usalama kwani Mgahawa wenyewe unafunguliwa wakati wa mchana.
Kati ya vinavyojumuishwa ni wanadensi ambao ni watoto wanaowatumbuiza wenzao na pia ma Dijei ambao pia ni watoto.
Zaidi ya watu 300 wakiwemo wazazi na watoto walihudhuria ufunguzi huo.
Mtindo huo umepata umaarufu katika miji miingine kama vile South Korea,Berlin na Los Angeles.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post