Kilabu ya watoto walio kati ya umri
wa miaka 6 na 12 ilifunguliwa rasmi katika mji wa New York wilaya ya
meatpacking nchini Marekani.
Mgahawa huo unaomilikiwa na kampuni
ya Cirkiz utakuwa ukifunguliwa mara moja kila mwezi kuwapa watoto fursa
ya kujivinjari mbali na vifaa vya kiteknolojia vilivyomo majumbani mwao.Laura lampart aliyekuwa ameandamana na mwanawe alisema kuwa kilabu hiyo ina manufaa kwani watoto walijihisi kama watu wazima na hakukuwa na tatizo la kuhofia usalama kwani Mgahawa wenyewe unafunguliwa wakati wa mchana.
Kati ya vinavyojumuishwa ni wanadensi ambao ni watoto wanaowatumbuiza wenzao na pia ma Dijei ambao pia ni watoto.
Zaidi ya watu 300 wakiwemo wazazi na watoto walihudhuria ufunguzi huo.
Mtindo huo umepata umaarufu katika miji miingine kama vile South Korea,Berlin na Los Angeles.