Header ads

Header ads
» » KITUO CHA TV NCHINI UGANDA CHAFUNGIWA BAADA YA KUONESHA PICHA ZA RAIS AKIWA AMESINZIA BUNGENI

Serikali ya Uganda imekifungia kituo kikubwa cha Televisheni cha nchi hiyo NTV kuripoti habari zozote zinazomhusu Rais baada ya kurusha hewani picha zinazomuonyesha Rais Yoweri Museveni amesinzia bungeni.
 
Mkurugenzi wa kituo cha habari za serikali Dennis Katungi amenukuliwa akisema: “Rais ana tabia zake wengi mnajua, huwa anatafakari na wanajua lakini bado wameonyesha picha hizo na kusema alikuwa amesinzia.”
 
Msemaji wa serikali Ofwono Opondo amethibitisha kuwa NTV Uganda itachukuliwa hatua za kinidhamu ambapo wameifungia kuripoti habari zozote zinazomhusu rais wakati bado serikali ikiangalia uhusiano wake na chombo hicho.
 
Ameituhumu NTV kwa kukosa utaalamu wa uandishi na kuegemea upande mmoja lakini hata hivyo hatua hiyo si ya kudumu ni ya muda tu kuwafanya wafikirie upya.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post