
Kampuni ya Facebook hivi karibuni imetangaza kuwa imefanikiwa kufanya
majaribio ya kwanza ya ndege isiyo na rubani iitwayo Aquila inayotumia
nishati ya jua.
Hivi sasa watu bilioni 4 hivi duniani bado
hawajaunganishwa na mtandao wa Internet. Mwaka 2014, kampuni hiyo
ilianzisha maabara ya uunganishaji, ambayo inalenga kutoa huduma ya
mtandao wa Internet kupitia ndege zisizo na rubani, satilaiti na mifumo ya mawasiliano ya simu
Tarehe 28 maabara hiyo ilifanya majaribio ya kwanza ya ndege ya Aquila
huko Arizona, Marekani. Kiunzi cha ndege hii kilitengenezwa kwa nyuzi za
kaboni, upana wa mabawa yake ni mkubwa kuliko ndege ya abiria ya Boeing
737, lakini uzito wake ni theluthi moja ya gari la nishati ya umeme.
Ndege hiyo inaweza kuruka angani kwa miezi mitatu mfululizo, lakini
inatumia nishati chache tu ambayo ni sawa na nishati inayotumiwa na
vyombo vitatu vya kukausha nywele au maikrowevu moja.
Kwa mujibu wa
mpango, ndege hiyo inaweza kuzunguka eneo lenye kipenyo cha kilomita 97,
na kutoa ishara ya mtandao wa Internet kutoka anga yenye urefu wa
kilomita 18 kwa mifumo ya mwangaza leza na mawimbi ya masafa ya
milimita.
Chanzo: technewstoday.com
Home
»
HABARI TECH
» Facebook yafanikiwa kufanya majaribio ya ndege isiyo na rubani inayotumia nishati ya jua
Topics: HABARI TECH
Imehaririwa na;- Unknown
Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
Playstore
TeknoTaarifa Video
TAARIFA ZILIZOSOMWA SANA
-
Shindano la kumsaka mrembo kutoka mkoa wa Kilimanjaro ambaye atakua akiuwakilisha mkoa huo kwenye shughuli mbali mbali za kijamii limezindul...
-
Ubuyu kama tulivyozoea wengine wanauweka rangi na sukari unatengenezwa vizuri tunafanya kula na kuna wengine ule unga wake hutengenezea...
-
Kwa mujibu wa mmoja wa wanafamilia ambae ameongea na Capital FM Nairobi, Mutula amekutwa akiwa amefariki dunia nyumbani kwake Macha...
-
TRA would like to recruit dynamic experienced and qualified personnel to fill vacant positions in the Research & Policy, Hum...
-
Huu ndo ujio mpya Rehema Chalamila aka Ray C baada ya ukimya wa muda mrefu kwenye muziki amerudi rasmi na hii singl...
-
Kama ni mpenzi wa vitu vikali na bora na umejipanga kuchukua Mzigo mpya wa Kompyuta mpakato “Laptopo” kwa Mwaka huu 2016,Ni...
-
Mitandao ya Intaneti inatumika na watu wa aina mbali mbali duniani kwa madhumuni tofauti tofauti. Kwa ufupi hapa leo tutaangalia matum...
Data Boosta