Kampuni ya Facebook hivi karibuni imetangaza kuwa imefanikiwa kufanya
majaribio ya kwanza ya ndege isiyo na rubani iitwayo Aquila inayotumia
nishati ya jua.
Hivi sasa watu bilioni 4 hivi duniani bado
hawajaunganishwa na mtandao wa Internet. Mwaka 2014, kampuni hiyo
ilianzisha maabara ya uunganishaji, ambayo inalenga kutoa huduma ya
mtandao wa Internet kupitia ndege zisizo na rubani, satilaiti na mifumo ya mawasiliano ya simu
Tarehe 28 maabara hiyo ilifanya majaribio ya kwanza ya ndege ya Aquila
huko Arizona, Marekani. Kiunzi cha ndege hii kilitengenezwa kwa nyuzi za
kaboni, upana wa mabawa yake ni mkubwa kuliko ndege ya abiria ya Boeing
737, lakini uzito wake ni theluthi moja ya gari la nishati ya umeme.
Ndege hiyo inaweza kuruka angani kwa miezi mitatu mfululizo, lakini
inatumia nishati chache tu ambayo ni sawa na nishati inayotumiwa na
vyombo vitatu vya kukausha nywele au maikrowevu moja.
Kwa mujibu wa
mpango, ndege hiyo inaweza kuzunguka eneo lenye kipenyo cha kilomita 97,
na kutoa ishara ya mtandao wa Internet kutoka anga yenye urefu wa
kilomita 18 kwa mifumo ya mwangaza leza na mawimbi ya masafa ya
milimita.
Chanzo: technewstoday.com
Home
»
HABARI TECH
» Facebook yafanikiwa kufanya majaribio ya ndege isiyo na rubani inayotumia nishati ya jua
Topics: HABARI TECH
Imehaririwa na;- Unknown

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
Soma na Hizi
Tangazo kwa Umma kutoka Wizara ya Elimu Sayanzi na Teknolojia
Serikali inatarajia kuajiri Fundi Sanifu wa Maabara ya Shule Daraja la II. Ajira hii ni kwa...Read more »
31Jan2017Ujumbe wa WhatsApp wamfikisha kizimbani Mwanafunzi Ardhi University
Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ardhi Dar es Salaam (ARU) Juvenal Shirima amepandishwa kizimbani aki...Read more »
28Jan2017Ujumbe wa Ndalichako kwa Tume ya sayansi na teknolojia (costech) Zanzibar
Waziri wa elimu, sayansi na teknolojia mhe: joyce ndalichako ameitaka tume ya sayansi na teknol...Read more »
27Jan2017Mabasi ya Abiria yasiyokuwa na dereva yaanza kutumika Paris Ufaransa.
Manispaa ya Paris imeanzisha utumizi wa mabasi yanayotumia umeme kusafirisha abiria kwa masafa ma...Read more »
24Jan2017Kituo cha utafiti wa kilimo Makutupora Mkoani Dodoma.chapiga hatua kwa Teknolojia ya uhandisi jeni (GMO)
KAMATI ya Taifa ya Matumizi Salama ya Bioteknolojia (NBC) imeridhishwa na matumizi ya...Read more »
24Jan2017Wanamazingira wazitaka serikali za Afrika kutumia Teknolojia ya nishati endelevu
Wanamazingira barani Afrika wamezitaka serikali za nchi za Afrika kuwekeza zaidi kwenye miradi...Read more »
24Jan2017

Playstore
TeknoTaarifa Video
TAARIFA ZILIZOSOMWA SANA
-
Mambo vipi Rafiki yangu? Kama wewe ni miongoni mwa...
-
Computer ina uwezo wa kufanya mambo ambayo binadamu...
-
Coca-Cola Kwanza Limited of Dar es Salaam, is part...
-
Si wengi wetu wanaofahamu umuhimu wa kula samaki mara...
-
The American Idol judge wore this eye popping red dress...
-
Kwa wale Rafiki zangu wa ma-gadgets and all...
-
Mambo vipi Rafiki zangu wasomaji wa Website hii, Siku...
Data Boosta
