Header ads

Header ads
» » Watumiaji wa Facebook Wataweza Kutumiana Pesa Kupitia ‘Facebook Messenger’

Facebook


M-Pesa bila ya shaka ni njia rahisi ya watu kutumiana pesa au kufanya malipo. Facebook wanaanzisha mtindo mpya wa kutumiana pesa kupitia programu yao ya jumbe ya Facebook Messenger itakayo muezesha mtumiaji kuunganisha akaunti yake na ile ya facebook.
Mfumo huo utaanzishwa nchini marekani kwa sasa na iwapo una kadi ya Visa au Mastercard utahitajika kubofa “$” kutuma pesa kwa umtakae kwenye mtandao wa facebook.
Facebook wanahakikishia watumizi wake kwamba mtindo huo ni salama kwa kusema: “Mbinu yetu ya malipo ni salama na inatumia miundombinu tofauti na mtandao wetu wa Facebook ili kuhakikisha malipo yanafuatiliwa kwa karibu.”
Pindi mtumizi atakapo ona alama ya “$” kwenyeMessenger yake, inamaanisha tayari yuko kwenye mtandao wa malipo ya Facebook.
Mtumizi atafinya alama hio na kueka kiwango cha pesa kisha kubofa ‘tuma’ kama anaetuma ujumbe. Pesa itatolewa moja kwa moja kutoka akaunti ya mtumizi na kuzituma kwa akaunti ya anayetumiwa.
Mtu atahitajika kueka maelezo zaidi kuhusu akaunti yake pamoja na kuwa na neno la siri ili kuzuia mtu kueza kutuma pesa bila idhini ya mwenye akaunti.
Mfumo wenyewe utaanza kutumika nchini Marekani kwenye kipindi cha wiki chache zijazo lakini unatarajiwa kuenea nchi nyengine duniani ambapo kutumiana pesa itarahisishwa na kupunguza gharamaya ada zinazolipishwa kama Western Union na Moneygram.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post