JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA
TANGAZO LA AJIRA
Jeshi la Polisi Tanzania linatangaza nafasi za ajira kwa mwaka wa
fedha 2015/2016 kwa vijana wenye elimu ya vyuo vya elimu ya juu,
waliosomea ujuzi/fani mbalimbali toka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali
na wahitimu wa kidato cha sita wa mwaka 2014 waliopitia Jeshi la Kujenga
Taifa kwa mujibu wa sheria. Wahusika watajaza fomu baada ya kujazwa
kikamilifu wataambatanisha vivuli vya vyeti na kutuma Makao Makuu ya
Jeshi la Polisi kwa njia ya Posta kabla ya tarehe 31/06/2015. Kwa anuani
ifuatayo:
Inspekta Jenerali wa Polisi,
Makao Makuu ya Polisi,
S.L.P. 9141,
DAR ES SALAAM.
SHAHADA
Maendeleo ya Jamii(Community development),Ushauri Nasihi [Counselling
Psychologist](2) Uchumi(Economy)(10)Ualimu(Education)(2)Menejimenti ya
Rasilimali watu(HRM), Utawala katika Utumishi wa Umma(Public
Administration)(3) Usimamizi na Utekelezaji wa Sheria[BaLE](12) Sheria
(LLB)(2) Uandishi wa Habari(2) Uhandisi Mitambo[Mechanical Engineer](5)
TV & Redio Production(5)Ugavi[BA In Procurement & Supplies](2)
Mazingira[BA in Environmental Disaster Mgt](5) Uchoraji[BA in Fine
Arts](5) Mkemia, Bailojia[Molecular Biology] (10)Kada za
Afya(10)Uhandisi Madini[Mining Engineer](5) Land Surveyor(2) Madaktari
wa Wanyama(5) Wataalamu wa Ujenzi Mafundi AC(2) Architecture(2) Quantity
Surveyor(2) Civil Engineer(2)
STASHAHADA
Utunzaji Kumbukumbu(30) Katibu Muhtasi[Personal Secretary](30)
Matengenezo ya kompyuta, Photocopy machines na Fax(10) Mafundi Mitambo
wa meli(2) Kada za Afya(5) Wataalamu Magari na Pikipiki Mafundi Umeme wa
Magari(5) Mafundi Magari(5) Manahodha(5) Ugavi(2) Mawasiliano[Diploma
in RadioCommunication](20) Madaktari wa wanyama(2) Land Surveyor
Cathographer (2) Mafundi AC(2) Wataalam ujenzi Hydro Geology Drilling
Well(2) Architecture Draftman(2) Civil Engineer(2)ASTASHAHADA(NTA level 3
or 4
Wataalamu Magari na pikipiki Mafundi Pikipiki(4) Mafundi Umeme wa
Magari(4) Mafundi Magari(4) Mafundi Rangi za Magari (Spray Painting)(4)
Madereva wa magari(50) Mafundi Unyooshaji wa Body (Panel Beating)(5)
Mafundi A/C(3) Mafundi Ushonaji (10)Wataalamu wa GIS Cathographer(2)
Land Surveyor(2) Madaktari wa Wanyama (3) Refridgeration & Air
Condition(2) Motor Rewinding(2) Wataalamu wa Ujenzi Welding &
Fabrication(2) Generator Maintenance(2) Electrical(3) Masonry (2)
Painting(3) Aluminium & Glass Work(2) Plumbing(2) Wataalamu wa
muziki Brass bandi (5) wood wind (5) String jazz (3) Percussive (2)
MASHARTI KWA MWOMBAJI
1. Mwombaji atajaza fomu ya maombi kikamilifu na atabandika
picha yake “Ppt Size” kwenye fomu.
2. Mwombaji aambatanishe katika fomu vivuli vya vyeti vyote
yaani cheti cha kuzaliwa, kuhitimu elimu ya sekondari[Leaving
& Academic], cheti/vyeti vya taaluma[Academic Transcript] na cheti cha
kumaliza Jeshi la kujenga taifa kwa wahitimu wa kidato cha sita.
3. Hati ya kiapo cha kuzaliwa haitakubalika.
SIFA ZA MWOMBAJI
1. Awe Mtanzania kwa kuzaliwa.
2. Awe na umri usiopungua miaka 18 na usiozidi miaka 25 kwa wahitimu wa
astashahada, stashahada na kidato cha sita.
3. Kwa wahitimu wa shahada awe na umri usiopungua miaka 18 na usiozidi
miaka 28.
4. Awe amehitimu chuo mwaka wa masomo 2014 tu.
5. Kwa wahitimu wa kidato cha sita awe amehitimu mwaka 2014 na kupitia
Jeshi la Kujenga Taifa kwa mujibu wa sheria
6. Awe na tabia njema.
7. Asiwe na kumbukumbu za kutenda uhalifu.
8. Awe na afya njema[kimwili na kiakili]
9. Awe hajaoa/hajaolewa au kuwa na mtoto.
10. Asiwe na alama za kuchora mwilini[tatuu].
11. Awe na urefu usiopungua sentimita 155 futi tano nchi mbili
12. Asiwe mtumiaji wa madawa ya kulevya.
13. Awe hajaajiriwa na idara nyingine Serikalini.
14. Awe tayari kuhudhuria mafunzo ya awali ya Polisi.
15. Awe tayari kufanya kazi popote ndani na nje ya Tanzania.
Imetolewa na
Makao Makuu ya Polisi(T)
DAR- ES- SALAAM.