Header ads

Header ads
» » Maelezo Mafupi ya nini cha kufanya ikiwa Simu yako imedondoka kwenye Maji

 Sony-Xperia-ZR-press- water resistant cell phone
Wengi  kwa sababu mbalimbai tumewahi kudondosha simu kwenye maji. Kwa watumiaji wa simu kudondosha simu ni suala la kawaida.
Kwa wengi baada ya kitendo hiki huwa tunajaribu kutafuta njia mbalimbali za kuokoa simu zetu ili zisiharibike zaidi.

Kwa hali ilivyo inawezekana simu kama kifaa isiwe tatizo pale inapodondoka, lakini muhimu ni zile taarifa zilizomo ndani ya simu.
Kuna uwezekano kwamba simu yako ilikuwa imewaka wakati inadondoka kwenye maji, kama maji yakiingia ndani mfumo wa umeme unaweza kuharibika kwa kupiga shoti. Sasa fuata hatua hizi
Zima simu yako
Ukishazima hatua muhimu inayofuata ni kutoa vitu vyote kwenye simu kama betri, kasha, kadi na vitu vingine ambavyo vinatumika kwenye matumizi ya simu yako. 
Itingishe
Tingisha simu yako juu na chini hasa sehemu za kuingiza umeme au kuchomeka kifaa cha kutoa picha au video au kifaa cha kuchomeka visikilizio na sehemu za kubonyeza.
Baada ya kutingisha tumia kitambaa laini , pamba au sponji kukausha maji yaliyopo kwenye simu yako kama yaliingia.
Iweke ndani ya mchele
Kama una mchele kwenye mfuko au chombo maalumu, iweke simu yako halafu funika kisha weka kwenye sehemu iliyokauka hii itasaidia kunyonya maji maji na mengine kwenye kifaa chako .

Acha simu yako ndani ya mchele kwa saa 24 mpaka 48, usijaribu kuiwasha au kuishika muda wote huo kuona kama imeanza kufanya kazi au la. Kama haikuwa na maji mengi ndani ya muda huo, itaanza kufanya kazi.
Weka akilini kwamba si lazima simu yako iwake baada ya kufanya yote hayo, kuna uwezekano wa asilimia 50 tu  wa simu yako kuwaka na kufanya kazi tena.
Peleka kwa mtaalamu
Kama imeshindikana kuwaka baada ya jitihada zote hizo ni vizuri upeleke kwa wakala aliyeidhinishwa  kuuza au kutengeneza simu husika kama umenunua kwake
Pamoja na maelezo yote hapo tu, unatakiwa ujiandae na ujue njia za kuikinga simu yako dhidi ya maji siku nyingine .
Kama unatembea sehemu za mvua au maji maji kama baharini, mto au bwawani unaweza kununua mfuniko usioingia maji kwa ajili ya kukinga simu yako
Mifuniko hii ina sehemu unayoweza kuangalia kama kuna simu imeingia, ujumbe au kitu kingine.
Suala la simu yako kuingiliwa na maji au kupata tatizo la umeme, mara nyingi halipo kwenye ‘warranty’  ili kuweza kupata faida ni bora kuwa na bima ya simu na vifaa vingine vya elekroniki ili inapopata shida iwe rahisi kupata nyingine kuliko kutumia gharama kubwa kununua kifaa kingine.
Muhimu ni kujua na kuzingatia suluhisho hili. Lakini njia nzuri zaidi ni kupeleka simu yako kwa fundi au mtaalamu wa simu ili aweze kuingalia na kufanya marekebisho kama kuna uwezekano huo.
Kuendelea kutumia simu mbovu au zenye shida fulani zinaweza kukuletea madhara ya kiafya, kwa sababu kuna vifaa ndani ya simu vinaweza kufanya kazi ndivyo sivyo. Vifaa hivi ni kama  kioo, mfumo wa sauti na mfumo wa umeme. Natoa tahadhari kwa watumiaji wa simu wenye mazoea ya kuchokonoa vifaa hivyo pasina ujuzi wowote. Hiyo ni kazi ya fundi.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post