
Meli ikiwa inazama na ikiwa imezungukwa na mitumbw pamoja na boti ambazo zilisaidia kwenye uokoaji
Makaburi ya Igoma ambako ndugu zetu waliokuwa wakisafiri kwa meli ya MV Bukoba walizikwa.
RIPOTI ya Tume ya Jaji Robert Kisanga, iliyochunguza chanzo cha ajali ya mv Bukoba, inasema usiku wa kuamkia siku ya ajali, meli hiyo ilipakia abiria kati ya 750 na 800 pamoja nawafanyakazi 37.Kati ya hao 114 waliokolewa wakiwa hai wakati 391 waliokolewa wakiwa wamefariki na kuzikwa katika makaburi ya Igoma nje kidogo ya Jiji la Mwanza.
Miili mingine ilichukuliwa na ndugu na jamaa kuzikwa kwao pia Jumla ya miili 332 haikupatikana.Kila mwaka ifikapo Mei 21 watu mbalimbali wakiongozwa na viongozi wa dini na mbalimbali kwenda eneo la makaburi na kufanya maombi kwa ajili kumbukumbu ya ndugu waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo.
Serikali ilishitaki aliyekuwa nahodha wa MV Bukoba, Jumanne Rume-Mwiru (sasa marehemu), Mkaguzi wa Mamlaka ya Bandari Gilbert Mokiwa, aliyekuwa Meneja wa Bandari ya Bukoba Alphonce Sambo, na aliyekuwa Maneja wa Bandari ya Kemondo, Prosper Lugumila.Kesi hiyo Na. 22 ya mwaka 1998, ilianza kusikilizwa Mei 14 mwaka 2001.
Miongoni mwa waendesha mashitaka katika kesi hiyo ni Eliezer Feleshi,ambaye kwa sasa ni Jaji wa Mahakama kuu ta Tanzania.Hukumu ya kesi ilitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Juxton Mlay (sasa mstaafu), Ijumaa, 29 Novemba 2002, majira ya saa sita mchana.Washitakiwa wote walishinda kesi, kufuatia hukumu ya kurasa 118 iliyosomwa kwa dakika 160 na Jaji Mlay kusema, MV Bukoba ilizama kwa sababu haikuwa na uwiano wa majini na siyo uzembe wa washitakiwa.
Serikali iliahidi kukata rufaa lakini hadi leo majaliwa ya rufaa hiyo hayajulikani na baadhi yawashitakiwa wamefariki dunia bila kujua hatma ya kesi hiyo wala stahili zao.
Kwa kipindi kirefu MV Bukoba ilikuwa ‘kaburi’ lenye kuelea katika Ziwa Victoria. Ilikwishapigwamarufuku kufanya safari kwa kuwa haikuwa na viwango vya ubora wa kuwa majini.
Meli hii ilijengwa na kampuni ya Kibelgiji na ikazinduliwa 27 Julai 1979. Siku ya uzinduzi, ilibainika haikuwa thabiti kwani ilikuwa inakosa uwiano.
Uongozi wa Kitaani Bongo news Blog unatoa pole kwa nduguna jamaa waliopoteza wapedwa wao kwenye ajali ya meli ya MV Bukoba.
Topics: MATUKIO
Imehaririwa na;- Unknown
Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
Playstore
TeknoTaarifa Video
TAARIFA ZILIZOSOMWA SANA
-
Matumizi mabaya ya simu ambayo yamekuwa yakifanywa na watoto wao kwa ajili ya kufanikisha michongo isiyo na tija, kampuni moja ya te...
-
Majambazi saba akiwemo mmoja ambaye amevalia sare za polisi wameiteka benki ya I&M jijini Dar es Salaam na kuchukuwa fedha z...
-
Matukio mengi yan a endelea kutokea yakiusishwa na Wanafunzi kutumia vibaya Mitandao ya Kijamii. Hii ni pamoja n a Wanafunzi wanne wa C...
-
Kampuni ya Google imetambulika kuwa bidhaa yenye thamani zaidi kwa mujibu wa shirika la fedha la linalojihusisha na ukaguzi wa thamani ya...
-
Baadhi ya watendaji wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), pamoja na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), ni miongoni mwa...
-
Watu waliojihami wameteka idadi ya watu wasiojulikana katika moja ya maduka makubwa mjini Nairobi leo. Watu 20 inaarifiwa wameuawa...
-
MATUKIO ya ukatili wa kutisha yanazidi kushika kasi kila kona ya nchi, safari hii h...
-
Wanasayansi waja na ngozi ya bandia inayoweza wekwa juu ya ngozi ya kawaida na kuonekana kama halisi, na huku ikiwa haiathiriwi na kulo...
-
Wanafunzi 7 wa kitivo cha uhandisi wa mashine cha chuo kikuu cha Uludag nchini Uturuki wamefanikiwa kuunda gari la kutumia nishati ya ...
Data Boosta