Header ads

Header ads
» » Bwana mmoja aliyemleta Kimada nyumbani kwake, wakati Mkewe hayupo, baada ya mkewe kurejea nyumbani ghafla.Hiki ndicho Alichofanya.

1 in 3 women are victims of relationship violence.

Bwana mmoja aliyealika msichana nyumbani kwake, wakati mkewe hayupo, alimkana msichana huyo na kumuita mwizi, baada ya mkewe kurejea nyumbani ghafla.
Bwana huyo, Kevin Gaylor wa Colorado Springs Marekani, alikutana na msichana kwenye mtandao wa Craiglist.com na kumwambia aende kumtembelea nyumbani kwake. Hata hivyo mke wa bwana Kevin alirudi nyumbani ghafla, na kumfaya bwana huyo kupagawa asijue la kufanya.
Muda mfupi baada ya mke wake kuwasili, msichana aliyealikwa naye akafika. Kujaribu kuokoa jahazi bwana huyo alipiga simu polisi na kusema kuna mwizi nyumbani kwake. Gazeti la Metro limesema polisi watano walikwenda haraka nyumbani kwa bwana Kevin kupambana na mwizi ambaye waliambiwa alikuwa na silaha.
Badala yake polisi walikuta msichana mwenye umri wa miaka 20 akiwa nje ya nyumba ya bwana Kevin. Msichana huyo aliwaambia Polisi kuwa alisafiri kwa muda wa zaidi ya saa moja ili kukutana na Kevin, na kuwa walikuwa wakiwasiliana kwa muda wa wiki mbili kupitia simu na internet. Polisi walipogonga mlango wa bwana Kevin, alitoka na kuanza kuzungumza kwa sauti ya chini na kuwasihi polisi wamuondoe msichana huyo. Hata hivyo bwana huyo alikamatwa na kushtakiwa kwa kosa la kutoa taarifa za uongo kwa polisi.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post