Kwa takribani kipndi kama cha mwezi mzima uliopita kumeibuka msuguano mkubwa sana hasa kwenye mitandao ya kijamii kati ya wafuasi wa CHADEMA dhidi ya wafuasi wa chama cha ACT.
Msuguano huo hasa unahusisha wale wafuasi wa CHADEMA kurusha tuhuma nzito dhidi ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA ndugu Zitto kwa kumuita -------, Anatumiwa na CCM kuuwa upinzani, Anaandaliwa mikutano yake na CCM na shutuma nyinginezo nyingi nyingi tu sina haja ya kuzirudia hapa.
Lakini kwa upande wa huyo aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA yeye alishapigia mstari kule alikokuwepo na ameanza safari yake mpya katika chama kipya na ambacho amakiasisi yeye mwenyewe wakati akiwa bado na kesi dhidi ya CHADEMA na hatukuwai kumsikia ama haijathibitishwa ya kwamba huko ACT alipohamia amekuwa akiwatuhumu ama kuwashambulia viongozi wa chama chake cha zamani lakini pia chama chake cha zamani.
Sasa nirudi katika hoja ya kwanini Mbowe, Slaa na baadhi ya wanachama wa chadema walio watiifu kwa Mbowe na wale wafuata mkumbo wanahofu dhidi ya ZITTO?
Ni ukweli usiopingika Mbowe na Zitto ndio waliotumia muda mwingi kukijenga chama hicho na kuwaaminisha Watanzania kwamba muarubaini wa matatizo yao umepatikana na katika pilika za kukujenga chama hicho ndugu Zitto aliwavutia vijana wengi sana kuipenda siasa hasa ikizingatiwa kipindi kile hakukuwa na vijana waliokuwa wanavutiwa na siasa.
Kwa mantiki hiyo ndani ya CHADEMA kuna viongozi wengi ambao wamekuwa wakinungunika muda mrefu sana kutokana na aina ya uongozi wa mabavu ambao mwenyekiti na katibu wake pamoja na wale vipenzi vyao wanaoutumia.
Na wamekuwa hawana sehemu ya kusema kwa kuwa wako ndani ya chama lakini wametengwa na ni wanamageuzi wa ukweli kabisa nikiwa na maana hawawezi kuhamia chama tawala kwa hiyo wamekuwa kwa muda mrefu wakivumilia vurugu zote na mabavu ya Mwenyekiti na genge lake.
Sasa hofu inakuja zaidi kwa Mwenyekiti na genge lake kwa kuwa wale Makamanda sasa wanamahali pakuelekea na hasa baada ya kuona mwanzo wa ziara za ACT na hali yakuwa Makamanda hao wanaushawishi mkubwa sana katika jamii inayowazunguka.
Wasalaam
Topics: MATUKIO
Imehaririwa na;- Unknown
Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
Playstore
TeknoTaarifa Video
TAARIFA ZILIZOSOMWA SANA
-
KAMATI ya Taifa ya Matumizi Salama ya Bioteknolojia (NBC) imeridhishwa na matumizi ya Teknolojia ya Uhandisi Jeni (GMO) yenye len...
-
Huu ndo ujio mpya Rehema Chalamila aka Ray C baada ya ukimya wa muda mrefu kwenye muziki amerudi rasmi na hii singl...
-
Makala hii inakupa maelekezo ya mambo adimu katika kusimamia barua pepe zako, ili kuboresha ufanisi na- kufurahia kuwa na akaunti ya ema...
-
Kuna taarifa kuwa chanzo cha kifo cha ghafla cha rapper Mangweir ni kuzidisha madawa ya kulevya aliyotumia usiku wa kuamkia leo. Inadaiwa ...
-
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Camilius Wambura alisema kuwa vijana watatu waliotoka Geita kuja jijini Dar es Salaa...
-
Kampuni moja ya Florida, Marekani imekuja na dhana ya kujenga meli ‘Freedom Ship’, itakayokuwa na uwezo wa kuwa na kila kitu ch...
-
Kampuni ya magari ya Honda yafahamisha kuliingiza sokoni gari lao lipyamwaka 2020 lililo na uwezo wa kujiendesha...
-
Lengo la TeknoTaarifa ni kukuletea Taarifa murua za Teknolojia kutoka sehemu mbalimbali, Huwezi kubisha nikikwambia kuwa, eneo hili la t...
Data Boosta
