Wanafunzi wa darasa la pili katika shule ya msingi Nyamarere mkoani Geita wakiwa darasani.
Wanafunzi katika shule zote mbili wanaishi katika
mazingira ya enzi za ujima kwani wengi wao wanasomea nje kutokana na
uhaba wa vyumba vya madarasa na baadhi yao chini ya miti ili kusaka
kivuli, wakati wale wanaopata fursa ya kuingia katika madarasa wanakalia
mawe kutokana na ukosefu wa maadawati.
Kuna nyakati ambazo wanafunzi wa madarasa mawili
au matatu wanalazimika kutumia chumba kimoja na hapo mwalimu akiingia,
huwafundisha walio wake kwa maana ya darasa husika na wale wa madarasa
mengine huwa watazamaji iwe kwa dakika arobaini au themanini za somo.
Shule ya Msingi Nyamarere yenye madarasa ya kwanza
mpaka sita, ina wanafunzi 742; wasichana 315 na wavulana 427 pamoja na
walimu 12. Shule hii ina madarasa mawili tu na ofisi moja ya mwalimu
mkuu ambayo pia hutumika kama maktaba na stoo.
Hii inamaanisha kuwa kwa idadi ya wanafunzi
waliopo, chumba kimoja cha darasa kinapaswa kukaliwana wastani wa
wanafunzi 371. Kwa upande wake, Shule ya Msingi Bweya yenye wanafunzi
401 ina vyumba vitatu, hivyo wastani wa wanafunzi katika darasa moja ni
134.
Niliwasili katika Shule ya Nyamarere muda wa saa
04:00 asubuhi na ilikuwa ni asubuhi tulivu huku anga likiwa limefunikwa
na mawingu yaliyoashiria kwamba huenda mvua ingenyesha siku hiyo.
Nilipokewa vyema na mwanafunzi aliyejitambulisha kwa jina la Neema Martine ambaye alinikimbilia baada ya kuniona.
Mwanafunzi huyo aliyeonyesha nidhamu ya hali ya
juu, aliniamkia kisha kunipokea mizigo yangu akiamini pengine kuwa mimi
ni mwalimu mpya.
Baada ya kusalimiana, Neema aliwaongoza wanafunzi
wenzake waliokuwa wameketi katika moja ya makundi mengi yaliyokuwa
katika eneo hilo la shule akisema: “Heshima kwa mwalimu toa.”
Wanafunzi walisimama na kupiga saluti wakisema kwa
pamoja: “Shikamaoo mwalimu”. Baada ya tukio hili waliketi na kuendelea
na kile ambacho walikuwa wakifanya, ambacho kwa wakati huo sikufahamu
kilikuwa ni kitu gani.
Kadiri nilivyokuwa nikiingia katika mazingira ya
shule hii ya Nyamarere nilianza kuhisi kwamba makundi kadhaa ya
wanafunzi niliowaona wakiwa wameketi nje, ni madarasa na walimu wao
walikuwa wakiendelea kufundisha.
Wapo waliokuwa wameketi sehemu za wazi, wengine
pembezoni mwa kuta za vyumba vya madarasa vilivyopo, wengine waliketi
chini ya miti mikubwa ya miembe na wengine walikuwa wakiendelea na
masomo katika boma la jengo ambalo halijaezekwa.
Topics: MATUKIO
Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
Soma na Hizi
Matukio yaliyojili katika ulimwengu wa Teknolojioa Mwaka 2016
MWAKA 2016 umefika ukingoni, kwanizimesalia saa chache kabla ya kuingia 2017. Ahsante kwa...Read more »
31Dec2016TCRA imeziagiza kampuni za simu kutenganisha vifurushi
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeziagiza kampuni za simu kuanzisha vifurushi vinavyote...Read more »
02Oct2015Facebook na UN washirikiana kutoa huduma ya bure ya Internet kwa wakimbizi wa Syria
Facebook na UN yashirikiana kutoa huduma ya bure ya Internet katika k...Read more »
01Oct2015Instagram yaweka rekodi mpya kwa kufikisha idadi kubwa ya watumiaji
Instagram yaweka rekodi mpya kwa kufikisha idadi kubwa ya watumiaji milion...Read more »
01Oct2015Umoja wa Ulaya na China kushirikiana katika utafiti wa 5G
Umoja wa Ulaya unasema kuwa ushirikiano huu utaongezea vituo v...Read more »
01Oct2015shule zote za Serikali kufungwa nchini Kenya
Serikali yatoa agizo la kwa shule zote kufuatia mgomo wa walimu...Read more »
20Sep2015

Playstore
TeknoTaarifa Video
TAARIFA ZILIZOSOMWA SANA
-
Mambo vipi Rafiki yangu? Kama wewe ni miongoni mwa...
-
Nabii Samwel Mahela wa Kanisa la...
-
Si wengi wetu wanaofahamu umuhimu wa kula samaki mara...
-
Computer ina uwezo wa kufanya mambo ambayo binadamu...
-
wakati huku kwetu bado wanafunzi wanaendeleza njia...
-
Kwa wale Rafiki zangu wa ma-gadgets and all...
-
Mambo vipi Rafiki zangu wasomaji wa Website hii, Siku...
Data Boosta
