Header ads

Header ads
» » Nimekuwekea taarifa ya Jamaa Aliyembaka Mtoto wa Miaka mitatu (3)


Wilson Saimon ‘Babu Nyemeni’ (21), mkazi wa Kijiji cha Mgeta wilayani Mvomero mkoani Morogoro aliyehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kudaiwa kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka mitatu.

DUSTAN SHEKIDELE-MOROGORO
USHIRIKINA? Katika hali ya kushangaza, Wilson Saimon ‘Babu Nyemeni’ (21), mkazi wa Kijiji cha Mgeta wilayani Mvomero mkoani Morogoro yamemkuta baada ya kuhukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kudaiwa kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka mitatu.

Mama wa mtoto aliyebakwa.

Babu Nyemeni anadaiwa kufanya unyama huo mwishoni mwa mwaka jana, nyumbani kwa Angel Bosco ambaye alikuwa amekwenda kuimba kwaya kanisani na kumuacha nyumbani mtoto huyo (jina tunalihifadhi) akiwa na mfanyakazi wake wa ndani.

Wilson Saimon akiwa mikononi mwa Polisi.

Akisoma hukumu ya kesi hiyo katika Mahakama ya Wilaya ya Morogoro, Hakimu Mkazi, Regina Futakamba alisema siku ya tukio mtuhumiwa huyo ambaye ni jirani yake Angel, alimuomba mtoto huyo kwa mfanyakazi wa ndani na kumwambia anakwenda kumnunulia pipi, mfanyakazi alimkubalia ndipo alipokwenda kumbaka kichakani, jambo ambalo mtuhumiwa huyo alilikiri mahakamani.

Alisema mtoto huyo alikutwa katika kichaka kilicho nje kidogo ya kijiji hicho akiwa analia kwa maumivu ndipo walipompeleka kwenye Zahanati ya Mgeta alikobainika alibakwa na kuharibiwa sehemu za siri.
Hakimu Regina alisema kutokana na kosa hilo, mtuhumiwa alitakiwa kufungwa kifungo cha maisha lakini alitoa nafasi kwa mtuhumiwa kujitetea ambapo alijitetea na hakimu kumpunguzia adhabu hiyo kwa kumfunga miaka 30 jela ili iwe fundisho kwa wengine.

Wakizungumzia tukio hilo, baadhi ya wananchi wa Mgeta walilihusishwa tukio hilo na imani za kishirikina kwani walisema walishangazwa na mtuhumiwa kumbaka mtoto mdogo kiasi hicho.
“Mh! Hii nahisi inawezekana kadanganywa na waganga kwamba atembee na mtoto mdogo ndiyo apate utajiri maana haya mambo nayo yapo,” alisema mkazi mmoja wa Kijiji cha Mgeta.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post