Header ads

Header ads
» » THIERRY HENRY AMETANGAZA KUSTAAFU KUCHEZA SOKA

Thierry Henry
Mshambuliaji wa zamani wa Klabu ya Arsenal na timu ya taifa ya Ufaransa Thierry Daniel Henry ametangaza kustaafu kucheza soka rasmi.
Nyota huyu alietwaa kombe la dunia mwaka 1998 akiwa na timu ya Ufaransa alijiondoa kwenye klabu yake New York Red Bulls mapema mwezi huu na kukawa na tetesi atachagua kujiunga na klabu nyingine kubwa barani ulaya.
" Napaswa kuwashukuru mashabiki wote, nawashukuru wachezaji wenzangu na watu binafsi wanaohusika na AS Monaco, Juventus, Arsenal FC, FC Barcelona,na New York Red Bulls na pia Timu ya taifa ya Ufaransa waliufanya wakati wangu wa mchezo kuwa Maalumu".
Henry alianza kuwika katika soka la kimataifa akianzia klabu ya Monaco kisha akaelekea Juventus ,kabla ya kutua Arsenal alikocheza kwa mafanikio makubwa.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post