Header ads

Header ads
» » Akamatwa kwa kumuuza mpwa wake Albino kwa Mganga wa kienyeji

Akamatwa kwa kumuuza mpwa wake zeruzeru Tanzania

Polisi wamkamata mtu aliyemuuza mpwa wake albino kwa mganga wa kienyeji

Polisi amkamata raia mmoja mwenye umri wa miaka 44 kwa kosa la kujaribu kumuuza mpwa wake ambaye ni zeruzeru kwa mganga wa kienyeji ili kupata utajiri.
Msemaji wa polisi kutoka mkoa wa Tabora alisema Margareth Khamis, mwenye umri wa miaka 6, alitekwa nyara siku chache zilizopita katika kijiji cha Kona nne  wilaya ya Nzega anapoishi na mama yake Joyce Mwandu na ndugu zake watatu.
Mwandu, alisema kundi la watu walioziba nyuso zao waliingia ndani ya nyumba yake na kumkamata binti yake na kukimbilia vichakani.
Juma Bwire, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, alisema operesheni ya kumkamata mtu aliyefanya kitendo hicho ilianza baada ya kupata fununu ya kusikia kwamba kuna mtu anataka kumnunua msichana huyo kwa bei waliyokubaliana.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka  huduma ya kwanza ilisema kuwa mganga huyo alikubali kulipia shilingi 75,000 kwa viungo vya zeruzeru huyo.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post