Header ads

Header ads
» » Kumbe Uchawi sio Kwetu tu, hata kwa wazungu hupo!


muuaji (kulia)akiwa  na wapelelezi nani ya pingu


KUUA  kwa shuku ya uchawi  kumefanyika nchini Uingereza kwa babu mmoja mwenye miaka 73 kumtia nyundo mwenzake mwenye umri wa 77.
babu huyo Alan Rogers baada ya kufanya mauaji hayo aliwapigia simu Polisi na kuwaambia amemuua jirani yake  Fred Hatch kwa kuwa anatumia uchawi kudhuru watu wengine.Wote hao ni wakazi wa Fair Oaks , Dinas Powys, Vale of Glamorgan.
Wakati akikamatwa na kutiwa pingu aliwaambia polisi kwamba amesubiri muda mrefu kumuua jirani yake huyo kwa kuwa ni mchawi.
Rogers amekiri kufanya mauaji asiyokudia alipofikishwa mahakama ya  Cardiff Crown Court, ambayo pia imekubali kwamba na alikuwa na utata katika afya ya akili yake wakati alipomshambulia Hatch. ugonjwa huo kwa kizungu unaitwa  paranoid schizophrenia.
Hata hivyo jaji  Warby  amemhukumu kuwa chini ya uangalizi wa watabibu maisha yake yote ili asidhuru wengine.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post