Katika harakati za kuboresha huduma zake, WhatsApp inadaiwa kujiandaa kuweka kitufe cha ‘‘Like’’ kama ilivyokuwa kwenye mtandao wa jamii wa Facebook.
Kulingana na tetesi zilizotolewa, kitufe hicho cha ‘‘Like’’ kitaweza kutumiwa wakati mtu atakapopokea ujumbe ambao hawezi kuujibu kwa muda ule.
Hivyo basi, mtumiaji ataweza kujibu kutumia kitufe cha ‘‘Like’’ ili kudhihirisha kuwa ameupokea kama ilivyokuwa katika matumizi ya alama za rangi ya buluu zinazoashiria kusomwa kwa ujumbe uliotumwa.